Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Contact Us
    • Privacy Policy
    Facebook Instagram YouTube
    Chikao Media
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • MAGAZETI YA LEO
    • TETESI ZA SOKA
    • BOXING
    • FORUM
    Chikao Media
    Home » CAF IMEISHA SASA TUNAREJESHA HESHIMA LIGI KUU
    KITAIFA

    CAF IMEISHA SASA TUNAREJESHA HESHIMA LIGI KUU

    By AdminFebruary 16, 2026No Comments2 Mins Read
    Share WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Telegram Email Copy Link
    Follow Us
    Facebook Instagram YouTube
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email Copy Link

    BAADA kuondolewa  katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika, Kocha Mkuu wa Simba SC, Steve Barker, ameweka wazi malengo yake mapya akiwataka wachezaji wake kuhamishia nguvu zote kwenye mashindano ya Ligi Kuu Tanzania Bara.

    Barker aliyasema hayo mara baada ya kumalizika kwa dakika 90 za mchezo wa mwisho wa hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Stade Malien, ambapo Simba iliibuka na ushindi wa bao 1-0 katika Uwanja wa Benjamin Mkapa  jijini Dar es Salaam.

    Licha ya ushindi huo, matokeo ya jumla hayakutosha kuiwezesha Simba kusonga mbele, jambo lililowafanya kuaga rasmi mashindano hayo.

    Barker amesema amefurahishwa na kiwango kilichoonyeshwa na wachezaji wake, akisisitiza kuwa ameona mabadiliko chanya na ukuaji mkubwa wa kikosi chake kadri mashindano yalivyokuwa yakiendelea.

    Kocha huyo ameeleza  kuwa sasa ni wakati wa kuangalia mbele na kujipanga upya kwa ajili ya malengo yaliyosalia ndani ya msimu huu, kuwa Ligi Kuu Tanzania Bara ni fursa muhimu kwa timu hiyo kurejesha heshima na kuonyesha ubora wao.

    “Tumeondolewa kwenye mashindano ya Ligi ya Mabingwa Afrika, lakini bado tuna Ligi Kuu Tanzania Bara. Tunakwenda kujiandaa vizuri na kupambana kutafuta matokeo chanya katika kila mechi,” amesema Barker.

    Ameongeza  kuwa dhamira yao ni kuhakikisha wanamaliza msimu wakiwa katika nafasi nzuri itakayowapa nafasi ya kushiriki tena Ligi ya Mabingwa Afrika msimu ujao, akiamini kuwa uzoefu walioupata msimu huu utakuwa chachu ya mafanikio yajayo.

    Follow on Facebook Follow on Instagram Follow on YouTube
    Share. WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Email Copy Link
    Previous ArticleVideo Mpya ya G Nako Inakumbusha Mashabiki Burudani ya Bongo Fleva
    Next Article UKWELI KUHUSU ISHU YA PENATI YA NAMUNGO

    Related Posts

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    April 3, 2026

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    April 3, 2026

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    March 31, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    Bernardo Apewa Thank You Rasmi Man City

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    Neymar amuachia Mungu kutoitwa timu ya Taifa

    “Nimehuzunika,Nimeumia lakini ndoto bado inaishi”Neymar Jr.

    © 2026 CHIKAO MEDIA | All Rights Are Reserved
    • Contact Us
    • Privacy Policy

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.