Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Contact Us
    • Privacy Policy
    Facebook Instagram YouTube
    Chikao Media
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • MAGAZETI YA LEO
    • TETESI ZA SOKA
    • BOXING
    • FORUM
    Chikao Media
    Home » ALI KAMWE: SIMBA YA SAFARI HII NI MBOVU SANA
    KITAIFA

    ALI KAMWE: SIMBA YA SAFARI HII NI MBOVU SANA

    By AdminSeptember 18, 2025No Comments2 Mins Read
    Share WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Telegram Email Copy Link
    Follow Us
    Facebook Instagram YouTube
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email Copy Link

    Ali Kamwe, Ofisa Habari wa Yanga SC amesema kuwa Simba SC ya msimu huu wa 2025/26  ni mbovu kuliko ile ya msimu uliopita wa 2024/25.

    Yanga SC kwa sasa mkononi wana taji la Ngao ya Jamii walitwaa kwa kushinda mbele ya Simba SC mchezo uliochezwa Uwanja wa Mkapa, Septemba 16 2025 ikiwa ni mchezo wa ufunguzi wa msimu mpya wa 2025/26..

    Baada ya dakika 90 ubao wa Uwanja wa Mkapa ulisoma Yanga SC 1-0 Simba SC, bao la ushindi likifungwa na Pacome dakika ya 53 akiwa ndani ya 18 alipomtungua Moussa Camara kipa namba moja wa Simba SC.

    Kamwe amesema: “Simba ya msimu huu ni mbovu zaidi kuliko ya msimu uliopita, ni mbovu kwa sababu wachezaji wapya hawana ubora wa kushindana naona wanapambana kutafuta matokeo uwanjani.

    “Kwa hali ilivyo ninaona kabisa ndoto yangu ya kufikisha furaha ya kumfunga Simba SC mara kumi mfululizo nazidi kuiona na kutwaa ubingwa wa ligi kwa mara nyingine tena,”alisema Kamwe.

    Kikosi cha Yanga SC kwa sasa kipo nchini Angola ambapo kipo hapo kwa ajili ya mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika ikiwa ni hatua ya awali.

    Yanga Ijumaa hii ya Septemba 19 watakuwa Uwanja wa Estadio 11 de Novembro wakicheza na Wiliete Sports Clube mechi ya awali Ligi ya Mabingwa Afrika.

    Mchezo huu unatarajiwa kuchezwa kuanzia saa 12:00 jioni ambapo Watanzania na dunia itashuhudia burudani hiyo  mubashara kupitia AzamSports1HD.

    Follow on Facebook Follow on Instagram Follow on YouTube
    Share. WhatsApp Facebook Twitter Pinterest Email Copy Link
    Previous ArticleHII HAPA RATIBA YA ANGA LA KIMATAIFA, AZAM FC, SIMBA, YANGA SC, SINGIDA BS
    Next Article SINGIDA BS YAANZA MAZOEZI YA KWANZA KIGALI, RWANDA

    Related Posts

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    April 3, 2026

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    April 3, 2026

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    March 31, 2026
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POSTS

    Bernardo Apewa Thank You Rasmi Man City

    Ujenzi wa Arena, Serikali Yatenga Bil400

    Selemani Mwalimu Yupo Anakuja, Mjiandae

    MSIGWA AELEZA SABABU ZA KUONGEZEKA GHARAMA UWANJA WA ARUSHA

    Neymar amuachia Mungu kutoitwa timu ya Taifa

    “Nimehuzunika,Nimeumia lakini ndoto bado inaishi”Neymar Jr.

    © 2026 CHIKAO MEDIA | All Rights Are Reserved
    • Contact Us
    • Privacy Policy

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.